Subscribe:

search

.

Sunday 5 August 2012

CHADEMA SASA KUANZA OPARESHENI SANGARA MOROGORO TAREHE 8


VIONGOZI, POLISI WAKUBALIANA UFANYIKE AGOSTI 8 KILOSA, FFU WAMWAGWA MITAANI KUDHIBITI WAFUASI
Venance George, Morogoro
BAADA ya mvutano wa siku mbili baina ya Jeshi la Polisi na Chadema kilichopanga kufanya mkutano mjini Morogoro jana, pande hizo mbili zilikubaliana kuwa mkutano wa kwanza ufanyike Agosti 8, mwaka huu Mikumi, wilayani Kilosa.
Makubaliano haya yanakuja kufuatia mazungumzo baina ya viongozi wa Jeshi la Polisi mkoani Morogoro na wale wa Chadema kuwa, kwa vile maonyesho ya Nanenane mkutano huo usongezwe mbele na ufanyike wilayani Kilosa Agosti 8, mwaka huu.
Awali Jeshi la polisi lilizuia kwa madai kutokana na kuwapo mgomo wa walimu nchini ambao ulisitishwa kwa amri ya mahakama Alhamisi iliyopita pamoja na kwamba, jeshi hilo halitakuwa askari wa kutosha na kusimamia matukio hayo.
Hata hivyo, kabla ya kufikiwa makubaliano jana hayo askari wengi wakiwagwa mitaani kudhibiti wafuasi wa Chadema kuandamana na kufanya mkutano wa hadhara.
Wakiwa na mabomu ya kutoa machozi, magari yenye maji ya kuwasha, silaha za moto na virungu, vikosi hivyo vilikabiliana na baadhi wafuasi hao kwenye mitaa mbalimbali mjini hapa na kufanikiwa kuwatia nguvuni baadhi yao.
Hali hiyo ilitokana na wafuasi hao kumiminika kwenye ofisi za Chadema mjini hapa kwa ajili ya kuandaa maandamano hadi kwenye Viwanja ambavyo walitarajia kufanyia mkutano wa hadhara.
Wafuasi hao wa Chadema pamoja na viongozi wa ngazi mbalimbali walishiriki kwenye vuguvugu hilo ambalo chama kimelipa jina Vuguvugu la Mabadiliko (M4C), licha polisi kutoa onyo kuwa wasithubutu kufanya maandamano na mikutano hiyo, kwa kile walichodai ni kutokuwa na askari wa kutosha wa kutoa ulinzi.
Jana asubuhi, Jeshi la polisi lilitawanya askari wake kwenye mitaa mbalimbali ya Mji wa Morogoro na barabara zote za kuingia na kutoka katika mji huo.
Magari yenye maji ya kuwasha pamoja na yale yaliyopakia askari wa FFU, yalionekana yaranda randa katika mitaa ya Mji wa Morogoro huku yakipeperusha bendera za rangi nyekundu kuashiria hali ya hatari.
Taarifa zilizopatikana mjini hapa zilidai kuwa vikosi hivyo vya askari zaidi ya 200 waliletwa hapa kutoka mikoa ya Dodoma na Dar es Salaam na kuungana na wenzao wa Morogoro.
Hata hivyo, hali hiyo haikuwaogofya wafuasi na wapenzi wa Chadema, kwani walionekana wakiendelea na maandalizi ya kujikusanya huku wengi wao wakiwa wamevaa sare na kubeba bendera za chama hicho.

Wafuasi hao walionekana wakiwa katika makundi kwa makundi wakielekea kwenye ofisi za wilaya za Chadema zilizoko Mtaa wa Kingo.
Hali hiyo iliwafanya baadhi ya polisi waliokuwa katika mitaa mbalimbali kuanza kuwakamata baadhi yao hususan pale walipoonekana kuwa katika makundi makubwa.
Kitendo hicho kiliibua jazba na kuwafanya baadhi ya wafuasi kutoa maneno makali ya kulilaani jeshi hilo.
Hali hiyo ilionekana kuwatia zaidi hamasa wafuasi hao ambao waliendelea kujikusanya kwa kwenye ofisi za chama huku wakihimiza kuwa waandamane na ikiwezekana wakabiliane na yeyote atakayewazuia.
Kutokana na sakata hilo,  polisi liliomba kukutana na viongozi wa Chadema wa mkoa na taifa ili kujadiliana nao.
Akizungumza na wafuasi na wanachama walifulika katika ofisi hizo baada ya majadiliano na polisi, Mkuu wa Operesheni za Chadema, Singo Benson Kigaila alisema kuwa, Jeshi la Polisi limewaomba kukubali kubadilisha ratiba na kupanga nyingine kadri chama hicho kitakavyopendekeza.
Aliongeza makubaliano yatakwenda sambamba kuwachia huru bila masharti wafuasi zaidi ya 10 walikuwa wamekamatwa pamoja na magari ya chama  hicho.
Alisema Jeshi la polisi limeomba maandamano na mkutano huo uliopangwa kufanyika jana usitishwe kupisha shughuli za maonyesho ya wakulima  ya Nane Nane, Kanda ya Mashariki  yanayofanyika kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere, mkoani hapa.

Alisema kuwa, kufuatia makubaliano hao waruhusiwa kufanya uzinduzi M4C kuanzia Jimbo la Mikumi, wilayani Kilosa Agosti 8 mwaka huu na kuendelea katika majimbo mengine tisa yaliyosalia.
Hata hivyo, Chadema imepanga kufanya mkutano mkubwa katika Jimbo la Morogoro mjini ambao utawahusisha viongozi wa kitaifa na wabunge Agosti 18, mwaka huu.
Kwa mujibu wa Chadema, maandamano hayo yatapambwa na watembea kwa miguu waliobeba mabango yenye ujumbe mbalimbali.www.mwananchi.co.tz

2 comments:

Anonymous said...

CCM watabana wataachia.hakuna kulala mpaka kieleweke

Anonymous said...

CCM watabana wataachia.hakuna kulala mpaka kieleweke