Friday, 31 August 2012
GAVANA AZINDUA MFUKO WA KUNUNUA DHAMANA
GAVANA wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Profesa Benno Ndullu akiongea na waandishi wa habari jijini Dar es salaam kuhusu masuala mbalimbali ikiwemo mfumo wa mawakala wa Benki hiyo wa kununua dhamana za Serikali na hati fungani kwa njia ya mtandano(online) kwenye mnada na hivyo kupunguza ule utaratibu wa dhamana wa kupeleka karatasi katika Benki ili kupata huduma hiyo.
Thursday, 30 August 2012
Tuesday, 28 August 2012
Monday, 27 August 2012
HUU HAPA MSIMAMO WA MNYIKA JUU YA VURUGU ZILIZOTOKEA MOROGORO
Niliwahi kutahadharisha baada ya tukio la Dkt Stephen Ulimboka kuwa serikali imeanza kutumia mbinu haramu kudhibiti fikra mbadala, CCM imeanza kuongoza serikali kiimla na ipo siku umma utafikia hatua ya kukiona kama chama cha mauaji. Raia watatu wasio na hatia wamefyatuliwa risasi na mmoja amefariki. Haya yamefanyika kwenye maandamano ya amani ya wananchi kuwapokea viongozi wa CHADEMA kuelekea kwenye mkutano. Vurugu zimeanzishwa na polisi kwa mujibu wa mashuhuda wa ushahidi wa video. Vyanzo vyangu vinaniambia sasa wameagiza gari tatu za FFU na gari za kuwasha toka Dar Es Salaam. Tuombe MUNGU wasiamue kuvuruga mkutano wa hadhara ambao wananchi wamekusanyika kwa wingi hivi sasa. States captured by grand corruption of the ruling party cronies for so many years resorts to bullets as a way of stopping M4C through the ballot. Maisha ya wachache yako mashakani lakini si mabadiliko kwa maslahi ya wengi.
John John MNYIKA,
27 Agosti, 2012
WAKULIMA WA MPUNGA KATAVI WANUSURIWA
WAZIRI MKUU Mizengo Pinda amewataka wakulima wa mpunga nchini kuanza kujipanga kuuza mchele nje ya nchi. Pinda alisema hayo juzi wakati akikagua kazi ya kuweka mitambo ya kinu cha kukoboa mpunga katika kata ya Mwamapuli na Majimoto wilayani Mlele mkoani Katavi, na ujenzi wa madaraja ya mto Msadya na mto Kavuo. Aliendelea kusema kuwa kulingana na mahitaji yatakayokuwepo, wakulima hao kama watajipanga vizuri wanaweza kuuza mchele watakaouzalisha hadi katika nchi za Burundi na Rwanda ambako soko la uhakika lipo. “Kwa mahitaji yatakayokuwepo, na kama wakulima watajipanga vizuri wanaweza kuuza mchele mpaka nchi za Rwanda na Burundi,” alisema Pinda kwenye taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa jana na ofisi yake. Aliendelea kufafanua kuwa kukamilika kwa mradi huo kutawasaidia wakulima kuuza mchele badala ya kuuza mpunga, ndipo alipoelekea Mwampuli kukagua kinu hicho kilichonunuliwa kwa fedha za Halimashauri kwa lengo la kuwasaidia wananchi wa kata hizo Kwa upande mwingine, diwani wa kata hiyo, Emmanuel Mponda alimweleza Waziri Mkuu kuwa kinu hicho kina uwezo wa kukuboa tani 300 kwa siku kikiendeshwa kwa saa nane kutwa nzima. Diwani huyo alieleza kuwa kinu hicho kina uwezo wa kuchambua mchele na kuupanga katika madaraja manne tofauti na kuufungasha kwa madaraja hayo, na kinatarajiwa kuanza kazi Septemba mara jenereta litakapokamlika kuunganishwa. “Mchele ukishakobolewa, unapangwa katika madaraja A, B, C, na daraja D zinakuwa ni chenga ambazo zitauzwa peke yake kwa ajili ya wauza vitumbua. Kinu hiki pia kina uwezo wa kutenganisha pumba kwa ajili ya mifugo na kuzipaki katika sehemu ya peke yake bila kuingiliana na uzalishaji wa mchele,” alisema Mponda. Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda Vijijini, Wilbroad Mayala alisema kinu hicho kimegharimu Sh96 milioni wakati jenereta la kuendesha kinu hicho lenye uwezo wa kuzalisha kilowati 120, limenunuliwa kwa sh86 milioni. Chanzo:mwananchi.co.tz |
PICHA MBILI ZA KIJANA ANAEDAIWA KUUWAWA NA POLISI HUKO MOROGORO KATIKA MAANDAMANO YA CHADEMA
Hizi ni baadhi ya picha za kijana anaedaiwa kuuwawa katika maandamano ya CHADEMA huko Morogoro.
NAPE AKATAA KUIOMBA RADHI CHADEMA
Akataa kuomba radhi, asema tuhuma atazithibitisha mahakamani, Amtaka Dk. Slaa kuandaa bilioni 3 na shilingi moja. Ni kwa kudai CCM inaingiza silaha nchini.
KATIBU wa Halmashauri Kuu ya Taifa Itikadi na Uenezi CCM, Nape Nnauye amewataka Chadema kwenda mahakamani haraka badala ya kusubiri kuombwa radhi kama walivyotaka ili kusafishwa dhidi ya madai ya chama chao kupewa mabilioni ya fedha na mataifa tajiri.
Aidha amemtaka Katibu Mkuu wa chama hicho Dk. Wilbrod Slaa kuiomba radhi CCM la sivyo itamburuza mahakamani kudai fidia ya sh. bilioni 3 na shilingi moja, kwa kuituhumu uongo kwamba imeingiza silaha kutoka nje ya nchi tena bila kulipia ushuru.
Nape alisema hayo leo Agosti 27, 2012, kwenye mkutano wake na waandishi wa habari, uliofanyika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, mtaa wa Lumumba mjini Dar es Salaam.
"Bila shaka mmesikia jana Chadema wakinitaka niombe radhi au wananipeleka mahakamani kudai fidia ya sh. bilioni 3, kwa madai eti nimesema Chama hicho kinapata mabilioni ya fedha kutoka kwa mataifa tajiri. Mkubwa hatishiwi nyau, nawataka waende haraka mahakamani wala wasisubiri hizo siku saba", alisema Nape.
Alisema, CCM inao ushahidi wa kutosha kuhusu madai aliyotoa Nape dhidi ya Chadema na kwamba huyo tayari kutoa uthibitisho huo mahakamani badala ya kuomba radhi.
"Nadhani wakienda mahakani itapendeza zaidi maana huko ndiko pazuri kutoa uthibitisho kuhusu tuliyosema, na ninawahakikishieni tukishathibitisha na Msajili wa Vyama akaupata uthibitisho huo chama chao kinafutwa", alisema.
Kuhusu CCM kumburuza Dk. Slaa mahakamani, Nape alisema, ameshawaagiza wanasheria wa Chama, kuandaa barua ya kusudio la mashitaka hayo, na Dk. Slaa atapelekewa ili aamue kama ataomba radhi au atakuwa tayari kwenda mahakamani.
"Wakati wanakwenda mahakamani, Chadema wamwambie babu yao ajiandae kuomba radhi au kuburuzwa mahakamani kuilipa CCM fidia ya sh. bilioni 3 na shilingi moja kwa kuizushia CCM uongo kwamba inaingiza silaha nchini tena", alisema Nape.
Bashir Nkoromo
Blogger & Senior Photojournalist
Uhuru Publications Ltd,
Publishers of Uhuru, Mzalendo and Burudani tabloids
Cell; +255 712 498008, +255 789 498008, +255 773 600007 +255 756 646131
E-mail: nkoromo@gmail.com, bnkoromo@yahoo.com.
P O Box 9221, Dar es Salaam.Tanzania, East Africa
POLISI WAWAPIGA MABOMU WAFUASI WA CHADEMA MOROGORO
Wafuasi wa chama cha demokrasia na maendeleo chadema
Askari waliokuwa katika eneo la tukio kabla ya kuanza kwa maandamano hayo
Moshi wa mabomu yaliolipuliwa kutawanya maandamano ya chadema leo mjini morogoro
Gari la chadema lililokuwa likiongoza maandamano hayo
HUYU HAPA NI MWENYEKITI WA CHADEMA JIJINI LONDON
ANAEONEKANA KWENYE PICHA NI CHRIS LUKOSI MWENYEKITI WA CHADEMA JIJINI LONDON. HAPO ALIKUWA ANAJIANDAA KUELEKEA KWENYE MKUTANO WA CHADEMA HUKO READING.
CHADEMA WAPATA WANACHAMA WAPYA 3,500 MKOANI MARA

Mwenyekiti wa Baraza la Vijana taifa wa Chadema(BAVICHA),John Hecheakigawa kadi mpya kwa wanachama wapya wa chadema

Mwenyekiti wa Baraza la Vijana taifa wa Chadema(BAVICHA),John Heche akionyesha baadhi ya kadi za wananchama wa CCM Wa
--
OPARESHENI maalumu ya ‘Vua gamba vaa Gwanda’ inayoongozwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), imeitikisa Wilaya ya Tarime mkoani Mara, baada ya zaidi ya wanachama 3,500 wakiwemo viongozi wa CCM kujiunga na CHADEMA wilayani hapa.
Mbali na idadi hiyo ya watu kujiunga na CHADEMA, pia wananchi wengi wamegombania kadi za chama hicho kama njugu, ikiwa ni lengo la kutaka kujiunga na harakati za vuguvugu la kutaka kuleta mabadiliko ya kisiasa hapa nchini kuelekea uchaguzi wa Serikali za mitaa mwaka 2014, na hatimaye uchaguzi mkuu mwaka 2015.
Wanachama hao wakiwemo viongozi wa CCM wamejiunga na CHADEMA wakati wa mkutano wa hadhara wa chama hicho, uliofanyika mjini Sirari kisha kuhutubiwa na mwenyekiti wa Baraza la Vijana taifa wa chama hicho (BAVICHA), John Heche.
Miongoni mwa viongozi wa CCM waliorudisha kadi kisha kukabidhiwa kadi za CHADEMA mkutanoni hapo, ni pamoja na mjumbe wa Serikali ya Kijiji cha Sirari, Masha Vincent ambapo mke wake pia Veronika Masha alirudisha kadi ya CCM kisha kujiunga na CHADEMA.
Akizungumza kwa niaba ya wanachama wengine wapya waliojiunga na chama hicho kikuu cha upinzani nchini mara baada ya kukabidhiwa kadi za Chadema, Masha alisema wamechukuwa uamuzi huo baada ya kuchoshwa na kile alichodai majungu, fitina na uhasama unaofanywa na baadhi ya viongozi wa CCM wilayani hapa.
Alisema, enzi za CCM zinaonekana kuelekea kuisha, hivyo kujiunga kwao na CHADEMA ni kuongeza vuguvugu la mabadiliko, na kuwaomba vijana kufanya maamuzi ya dhati katika kuleta mabadiliko ya kisiasa, kijamii na kiuchumi.
“Mimi nimeamua kuondoka rasmi CCM. Maana yupo kiongozi mmoja hapa Sirari alikuwa anatusakama baada ya kumpinga mambo yake. Sasa tupo kwenye chama makini na chenye mtazamo mpana katika maendeleo ya nchi hii”, alisema Masha kisha kushangiliwa na umati mkubwa wa watu.
Awali, mwenyekiti wa Bavicha taifa, John Heche aliwaomba Watanzania kutumia kura zao vizuri uchaguzi wa serikali za mitaa wa mwaka 2014 pamoja na uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani utakaofanyika nchini mwaka 2015 kwa kuipigia kura CHADEMA ili ishike dola na kuleta mabadiliko ya kweli katika maendeleo ya wananchi.
Alisema, CHADEMA imedhamiria kuleta ukombozi mpya kwa wananchi wa taifa hili, na kwamba iwapo Watanzania wataiwezesha kuingia madarakani mwaka 2015, itahakikisha serikali yake inatumia vizuri rasilimali za nchi kwa faida ya Watanzania wenyewe na si wawekezaji.
Aidha, akiwa katika mkutano wa hadhara kule Muriba Tarime jana, Heche alilaani vikali mauji ya vijana yanayodaiwa kufanywa na baadhi ya askari polisi katika mgodi wa dhahabu wa Nyamongo uliopo wilayani hapa, na kusema upo uwezekano wa kuishtaki serikali ya Tanzania katika mahakama ya Kimataifa ya makosa ya uhalifu (ICC), kuhusiana na mauaji hayo.
Alisema, CHADEMA haiwezi kuendelea kuona Watanzania wanauawa kama wanyama katika wilaya hiyo, hivyo ikibidi ipo siku serikali italazimika kwenda kujibu mashtaka kwenye mahakama hiyo ya ICC kuhusiana na unyama inaowafanyia wananchi wake kwa kuruhusu jeshi lake la polisi kutumia mtutu kuwaua raia mgodini hapo.
“Hatuwezi kukubali vijana wetu, Watanzania wenzetu, wakurya wenzetu waendelee kuuawa kwa kupigwa risasi na polisi katika mgodi wa Nyamongo. Ipo siku serikali ikibidi itashtakiwa ICC kutokana na mauaji ya wananchi wetu”, alisema mwenyekiti huyo wa Bavicha taifa, Heche.
Alisema, mgodi wa Nyamongo kama ungelitumiwa vizuri na Serikali ya CCM ingelisaidia kupeleka maendeleo ya elimu, barabara, maji safi na salama ya kunywa, hospitali pamoja na mawasiliano, lakini kwa sasa madini hayo yanatumika kuwanufaisha raia wa nje ya nchi.
Hata hivyo, aliituhumu Serikali ya CCM kupitia kwa Rais Jakaya Kikwete kwamba utawala huo umekuwa ombaomba namba moja kwa misaada huko Ulaya, na kusema wakati mwingine Rais Kikwete huwa anapishana na ndege za wazungu zikiwa zimebeba madini, huku kiongozi huyo naye akitoka Ulaya kuomba vyandarua, jambo ambalo litaenda kudhibitiwa na CHADEMA itakapoingia Ikulu 2015.
Chanzo: Hakingowi.com
Sunday, 26 August 2012
KAMATI KUU YA CCM YAWAPONGEZA BAADHI YA MAWAZIRI WAKE
Raymond Kaminyoge KAMATI Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (CC), imewapongeza mawaziri kwa kuchukua hatua dhidi ya watendaji wanaotuhumiwa kwa vitendo vya matumizi mabaya ya ofisi za umma wakiwamo wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) na Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) na kuwataka waendelee na kasi hiyohiyo. Pongezi hizo za Kamati Kuu zimetolewa baada ya kikao chake kilichofanyika Ijumaa iliyopita na zimekuja baada mawaziri kadhaa kuwachukulia hatua za kinidhamu baadhi ya watendaji walio chini ya wizara zao kwa tuhuma mbalimbali. Mawaziri waliowachukulia hatua watendaji ni pamoja na Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe, Waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamis Kagasheki, Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo na Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk Abdallah Kigoda. Juzi, Kamati Kuu iliipongeza Serikali kwa kutekeleza maagizo yake ya kutaka ichukue hatua dhidi ya watendaji waliohusishwa katika ubadhilifu katika mashirika ya umma. “Kamati Kuu inawapongeza mawaziri walioanza kutekeleza maagizo hayo kwani mwisho wa siku maisha bora kwa kila Mtanzania yatawezekana,” ilisema taarifa iliyotolewa jana na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye. Kamati Kuu ilieleza katika taarifa yake kuwa ipo haja ya kuwachukulia hatua watendaji wakuu wa mashirika yaliyohusishwa na ubadhirifu mbalimbali na kwamba kitendo hicho cha mawaziri hao ni kutekeleza agizo lake. Mei 17, mwaka huu, Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk Kigoda alimsimamisha kazi Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Charles Ekelege ili kupisha uchunguzi wa tuhuma zilizokuwa zikimkabili. Miongoni mwa tuhuma hizo ni pamoja na kuyapa zabuni kampuni hewa za ukaguzi wa magari kabla hayajaingia nchini. Muda mfupi baadaye, Juni 5, mwaka huu, Dk Mwakyembe alimsimamisha kazi Kaimu Mtendaji Mkuu wa Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), Paul Chizi kutokana na tuhuma mbalimbali. Hivi karibuni, pia Dk Mwakyembe alisimamisha kazi Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Ephraim Mgawe, wasaidizi wake wawili na Meneja wa Bandari ya Dar es Salaam, Cassian Ng'amilo kupisha uchunguzi wa wizi wa vitu mbalimbali yakiwemo makontena 40 ya vitenge katika Bandari ya Dar es Salaam. Pia aliwasimamisha kazi Meneja wa Kituo cha Mafuta ya Ndege Kurasini (Kurasini Oil Jet - KOJ), Meneja wa Kituo cha Mafuta JET na mhandisi wa mafuta wa kituo hicho, baada ya kubainika kuwepo kwa wizi wa mafuta. Waziri Kagasheki kwa upande wake, alimfukuza kazi Mkurugenzi wa Wanyamapori, Obeid Mbanga kwa kashfa ya kusafirisha wanyama kwenda nje ya nchi. Julai 14, mwaka huu, Bodi ya Tanesco ilimsimamisha kazi Mkurugenzi Mtendaji wa shirika hilo, William Mhando ikielezwa kuwa ni maelekezo ya Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Muhongo ili kupisha uchunguzi wa matumizi mabaya ya madaraka katika ofisi yake. Mbali na kupongeza kazi hiyo, pia CC ilizungumzia mgogoro wa Tanzania na Malawi. Kuhusu hilo, Nape alisema Kamati Kuu imewatahadharisha wanasiasa na vyombo vya habari vinavyochochea vita na uhasama kati ya nchi hizo mbili. “Kamati Kuu imetaka suala hilo kuiachia diplomasia ichukue mkondo wake na Serikali iushughulikie na kuumaliza mgogoro huo,” alisema Nape. Pia, ilipokea taarifa ya maendeleo ya uchaguzi ndani ya chama na kusema imeridhishwa na maendeleo hayo ya uchaguzi na kuagiza kila kikao husika kihakikishe haki inatendeka hasa katika uchujaji wa majina Chanzo:Mwananchi.co.tz |
NAIL Armstrong BINADAMU WA KWANZA KUFIKA MWEZINI AFARIKI DUNIA
NAIL Armstrong linaweza lisiwe jina maarufu enzi hizi, lakini hilo ndilo jina lililoshika chati mwishoni mwa miaka ya 1960 kwani alikuwa binadamu wa kwanza kukanyaga mwezini.Hata hivyo gwiji huyo wa mambo ya anga , amefariki akiwa na umri wa miaka 82 akiacha rekodi yake hiyo iliyotikisa dunia. Neil Armstrong alitua mwezini Julai 20, 1969 akiwa katika chombo kilichoitwa Apollo na kusema ''hiyo ilikuwa hatua ndogo ya binadamu, lakini mapinduzi makubwa kwa ubinadamu''. Armstrong na mwanaanga mwenzake Buzz Aldrin walitumia saa mbili na nusu wakitembea juu ya mwezi . Neil Armstrong na wanaanga wenzake watatu Novemba mwaka 2011, walitunukiwa tuzo ya Congressional Gold Medal ambayo ndiyo ya juu zaidi inayotolewa kwa raia nchini Marekani. Armstrong amefariki dunia jana katika hospitali ya Columbus jimboni Ohio ambako alifanyiwa upasuaji wa moyo mapema mwezi huu. Kulingana na wasifu wa Armstrong ambao umechapishwa na Shirika la Anga la Marekani, NASA, mwanaanga huyo aliyezaliwa jimboni Ohio mwaka 1930, alisafiri kwa ndege kwa mara ya kwanza akiwa na miaka sita, na kupata leseni ya kuendesha ndege akiwa na miaka 16, hata kabla ya kujua kuendesha gari. Alitumikia Jeshi la Marekani kama rubani wa ndege za kivita wakati wa vita vya Korea, na baadaye akajiunga na masomo ya sayansi ya anga. Baadaye aliajiriwa kama rubani wa kuzifanyia ndege majaribio. Neil Armstrong alijiunga na programu ya anga mwaka 1962, na kurusha chombo cha kwanza cha anga miaka minne baadaye. Aliteuliwa kuwa kiongozi wa wanaanga walioshiriki katika safari ya Apollo, ambayo iliwafikisha wanadamu wa kwanza mwezini. Hatua yake ya kwanza mwezini iliangaliwa na mamilioni ya watu duniani kwa njia ya televisheni.Baada ya kutangazwa kwa kifo cha mwanaanga huyo, Mkuu wa Shirika la Anga la Marekani, NASA, Charles Bolden ametuma salamu zake za rambirambi kwa familia ya Armstrong.Charles Bolden amesema wakati wowote kutakapokuwa na vitabu vya historia, jina la Neil Armstrong litaandikwa kwenye kurasa za vitabu hivyo. Amesifia jinsi Neil Armstrong alivyoishi maisha ya unyenyekevu, na kusema kuwa mfano wake ni wa kuigwa. Pia Rais Barack Obama wa Marekani ametoa salamu za rambirambi zake, na kusema mwanaanga huyo ni miongoni mwa mashujaa wakubwa wa Marekani.Amesema Armstrong pamoja na wenzake 11 katika chombo cha Apollo, walibeba matarajio ya taifa zima la Marekani katika safari yao ya anga mwaka 1969. ''Waliionyesha dunia ari ya Marekani kuangalia mbali zaidi ya yale yanayofikirika, na kuthibitisha kuwa penye juhudi na maarifa, kila kitu kinawezekana,'' amesema Obama, na kuongeza kuwa ujumbe alioutoa Armstrong baada ya kukanyaga kwenye ardhi ya mwezini, ni mafanikio ya binadamu ambayo kamwe hayatasahaulika. Katika tangazo lililotolewa na familia ya Armstrong kufuatia kifo chake, mwanasayansi huyo ametajwa kuwa shujaa wa Marekani, ambaye muda wote yeye alisisitiza kuwa alichokifanya kilikuwa wajibu wake kikazi. Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa Familia yake imesema kuwa kifo chake kimetokana na matatizo yaliyofuatia upasuaji wa moyo. Familia ya Armstrong imesema kuwa mwanaanga huyo aliendelea kufuatilia maendeleo ya safari za anga, na kila alipofanya hivyo shauku yake ya ujana ilijitokeza tena. Neil Armstrong alistaafu kutoka NASA mwaka 1971 na alifanya kazi kwenye bodi ya wakurugenzi. Hakupenda kuwa mtu wa kujionyesha onyesha, isipokuwa mara chache tu kwenye kumbukumbu za safari ya kwanza mwezini, au akiunga mkono kuendelea kwa utafiti wa anga. Familia yake imesema kuwa, ingawa Neil Armstrong alipenda kuishi maisha yake bila bugudha, alifurahia ujumbe wenye nia njema kutoka kila pembe ya dunia kuhusu yeye na wenzake Chanzo:Mwananchi.co.tz |
Subscribe to:
Posts (Atom)






