Subscribe:

search

.

Saturday 18 August 2012

RAIS KIKWETE AREJEA NYUMBANI

 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Inspekta Jenerali wa Polisi Saidi Mwema baada ya kuwasili  usiku huu Agosti 19, 2012 kutoka Maputo, Msumbiji alikohudhuria kikao cha viongozi wa Jumuiya Ya Maendeleo Kusini Kwa Afrika (SADC) uliofunguliwa tarehe Agosti 17,  2021 na kumalizika jana jioni  Agosti  18 2012. Katika kikao cha Jana Tanzania imechukua uenyekiti wa Kamati ya Siasa, Ulinzi na Usalama kutoka Afrika ya Kusini ambapo uenyekiti wa SADC umechukuliwa na Msumbiji kutoka Angola. Nafasi hizi ni za mwaka mmoja mmoja
  
 Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiwa na Mkuu wa Wilaya ya Temeke Mhe Sophia Mjema baada ya kuwasili  usiku huu Agosti 19, 2012 kutoka Maputo, Msumbiji alikoambatana na Rais Kikwete katika  kikao cha viongozi wa Jumuiya Ya Maendeleo Kusini Kwa Afrika (SADC) uliofunguliwa tarehe Agosti 17,  2021 na kumalizika jana jioni  Agosti  18 2012. Katika kikao cha Jana Tanzania imechukua uenyekiti wa Kamati ya Siasa, Ulinzi na Usalama kutoka Afrika ya Kusini ambapo uenyekiti wa SADC umechukuliwa na Msumbiji kutoka Angola. Nafasi hizi ni za mwaka mmoja mmoja.

PICHA NA IKULU

0 comments: