Subscribe:

search

.

Wednesday 15 August 2012

Watakiwa Kufukuzwa Nchini Kama Hawatailipa Serekali Mrahaba




Na: Mahmoud Ahmad Arusha

Serekali imetishia kuwatimua wawekezaji wa kampuni ya madini ya Tanzanite one iliyopo Mererani wilayani Simanjiro iwapo watashindwa kulipa deni la zaidi ya dola za kimarekani milioni 2.2 zilizotokana na ukwepaji kodi .

Katibu mkuu wizara ya nishati na madini Eliakim Maswi alitangaza msimamo wa serikali wa kupitia upya mikataba ya makampuni ya madini hapa nchini baada ya kugundulika kuwa yapo makampuni kadhaa yamekuwa yakiendesha shughuli zake za madini bila kulipa ushuru wa serikali kinyume cha sheria.

Akizungumza na chama cha wanunuzi na wauzaji wa madini nchini TAMIDA,jijini Arusha jana,Maswi alisema kuwa kampuni ya Tanzanite one imekuwa ikikwepa kulipa kodi ya mrahaba wa madini tangu mwaka 2004 hadi 2008 na kufikia kiasi cha shilingi bilioni 3.4 fedha za kitanzania.

Alisema kuwa kampuni hiyo ilikuwa ikitumia ujanja wa kukwepa kulipa mrabaha wa mauzo pale inapokuta soko la madini nje ya nchi limeongezeka na kwamba serikali kupitia kitengo cha ukaguzi wa madini iliweza kubaini ukwepaji huo wa kodi na kuiamuru kampuni hiyo kulipa kiasi hicho cha fedha au ifungashe virago.

‘’tulibaini ukwepaji wa ulipaji kodi kwa kampuni ya Tanzanite one baada ya kuanzisha kitengo maalumu za ukaguzi wa migodi hapa nchini na tulipoifikia kampuni hiyo ndipo tulipobaini imekwepa kulipa kodi kiasi hicho,na hivi sasa tunaanza kupitia upya ikataba ya makampuni ya madini’’alisema Maswi

Aidha alifafanua kuwa kampuni hiyo iligoma kulipa deni hilo ikidai ni kubwa sana ,ndipo serikali ilipotaka kufanya ukaguzi upya ,kupitia wakaguzi wake , lakini kampuni hiyo iligoma na kudai kuwa ipo tayari kulipa deni hilo .

Aliongeza kuwa iwapo kampuni hiyo ingegoma kulipa deni hilo serikali ilikuwa tayari kuwatimua na kuwamilikisha wazawa mgodi huo.

Kwa mujibu wa kamishina wa madini kanda ya kaskazini Benjamin Mchwampaka alisema kuwa tayari kampuni hiyo imeshaanza kulipa deni hilo na kwamba hadi sasa imeshatoa malipo ya dola 200,000 zaidi ya fedha za kitanzania milioni 310,huku serikali ikiitaka kuhakikisha inamaliza kulipa deni hilo hadi kufikia jamuari mwaka 2013.

Hata hivyo katibu huyo aliitaka TAMIDA kuisaidia serikali kuyafichua makampuni yanayokwepa kulipa ushuru wa madini wakiwemo baadhi ya wafanyabiashara wakubwa ili wachukuliwe hatua na kusisitiza kuwa kwa sasa serikali imeanza mkakati wa kupitia upya mikataba ya makampuni ya madini hapa nchini.
Chanzo:mjengwablog.com

0 comments: