Subscribe:

search

.

Tuesday 16 October 2012

MKUTANO WA UTALII WAFANYIKA ARUSHA


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akihutubia alipofungua Mkutano wa kwanza wa Kimataifa wa Kutangaza Utalii kwa Nchi za Bara la Afrika na Kuhamasisha Utalii Endelevu
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal (kushoto) akipokea barua ya wazi kutoka kwa Katibu wa Mkuu wa Shirika la Utalii la Dunia, Taleb Rifai, iliyotolewa na Baraza la Waendesha Utalii Duniani (WTTC) mara baada ya kufungua Mkutano wa Kuhamasisha utalii barani Afrika leo, Oktoba 15, 2012, jijini Arusha. Katika Mkutano huo pia umehudhuriwa na Mawaziri 17 kutoka nchi mbalimbali za Afrika
 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipunga mkono kuwaaga wasanii wa ngoma ya asili wa kabila la kimasai wakati akiondoka katika ukumbi wa mikutano wa AICC jijini Arusha leo Oktoba 15, 2012 baada ya kufungua mkutano wa kwanza wa Kimataifa wa Kutangaza Utalii kwa Nchi za Bara la Afrika na Kuhamasisha Utalii Endelevu katika nchi hizo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiangalia Pakti ya kifuko cha unga wa Ubuyu na kusikiliza maelezo kutoka kwa Meneja Masoko na Mauzo wa kampuni ya Moringa Consultancy (TZ) Co Ltd, Christina Ngoti, wakati Makamu alipokuwa akitembelea Mabanda ya Maonyesho baada ya kufungua mkutano wa kwanza wa Kimataifa wa Kutangaza Utalii kwa Nchi za Bara la Afrika na Kuhamasisha Utalii Endelevu katika nchi hizo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa Mtaalam wa Tiba za Asili, James Kangaa, wakati Makamu alipokuwa akitembelea Mabanda ya Maonyesho baada ya kufungua mkutano wa kwanza wa Kimataifa wa Kutangaza Utalii kwa Nchi za Bara la Afrika na Kuhamasisha Utalii Endelevu katika nchi hizo.

0 comments: