Subscribe:

search

.

Wednesday 3 October 2012

RAIS JK AONGOZA UJUMBE WA TANZANIA KATIKA MKUTANO NA KATIBU MKUU WA UMOJA WA MATAIFA BAN KI MOON.


 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na waandishi wa habari hawapo pichani, wakati wa uzinduzi wa mpango wa pili wa  Ubunifu wa Uboreshaji wa  Huduma za  Afya ya Mama na Mtoto, katika maeneo ya vijijijni Nchini  Tanzania, mpango  huo  wa   miaka mitatu unafadhiliwa na wafadhili wawili, Meya ya Jiji la New York na  philanthropies Michael Bloomberg na Dr. Helle Agerup ambapo wamechangia dola za kimarekani milioni 15 kutoka kushoto ni Meya wa jiji la New York Michael Bloomberg, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon, Rais Jakaya Mrisho Kikwete,  na Dr, Helle Agerup
  Meya Michael Bloomberg, Ban Ki Moon, Rais  Jakaya Kikwete na Dr. Hellen wakiangalia video fupi iliyokuwa ikionyesha kazi zilizofanywa za ukoaji wa  akina mama wajawazito kwa kuwapatia huduma ya upasuaji wa dharura, huduma ambayo imepatika kwa ufadhili wa  Meya na   Philanthropies Michael Bloomberg ambapo kwa kupitia ufadhili alioufanya kuanzia mwaka 2006 zaidi ya wataalam 106 wakiwamo wakunga na manesi wamepatiwa mafunzo ya upasuaji wa dharura, pia huduma za afya zimeboreshwa kwa kujenga au kuvifanyia ukarabati vituo vya afya na zahanati katika ngazi za vijiji katika  maeneo ya  mikoa ya Pwani, Morogoro na Kigoma. Ufadhili  na kazi kubwa iliyofanywa na  Bloomberg   pamoja na juhudi za   Rais Jakaya Kikwete zimemvutia Dr. Hellen naye kuwekeza nchini Tanzania.

 Rais  Jakaya Kikwete akisaini kitabu cha wageni anayetizama pembeni ni Katibu Mkuu  Ban Ki Moon

Rais  Jakaya Kikwete akiongoza ujumbe wa Tanzania katika  mazungumzo yake na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa  Ban Ki  Moon ambaye naye aliongoza ujumbe wake. Matukio hayo yote yamefanyika siku ya  Jumanne katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa,  Jijini New York, Marekani.

Chanzo:Mjengwa.blogspot.com

0 comments: