Waziri wa ujenzi Dkt. John Pombe Magufuli akikagua kipande cha barabara (kilometa 33) zinazorudiwa kujengwa kwa kiwango cha lami na kampuni ya CHICO ambayo inadaiwa awali kuijenga chini ya kiwango. Kampuni ya CHICO inajenga kipande hicho kwa gharama zake pamoja na mkandarasi mshauri. Gharama ya ujenzi wa kipande hicho kinachoanzia katika kijiji cha Misigiri hadi Shelui ni zaidi ya shilingi bilioni 80.

Meneja wa TANROADS mkoa wa Singid Mhandisi Yustaki Kangole akitoa taarifa yake ya ujenzi wa kipande cha barabara kinachoanzia kijiji cha Misigiri hadi Shelui kilometa 33. Kipande hicho kinarudiwa kujengwa na kampuni ya kichina CHICO baada ya awali kukijenga chini ya kiwango.

Waziri wa ujenzi Dkt. John Pombe Magufuli (wa kwanza kushoto) akiwa na mkuu wa mkoa wa Singida Dkt. Parseko Kone (katikati) na Mkuu wa wilaya ya Iramba Yahaya Nawanda (wa kwanza kulia). Muda mfupi kabla ya waziri Magufuli kuzungumza na wafanyakazi wa kampuni ya CHICO.

Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wafanyakazi (hawapo kwenye picha) wa kampuni ya CHICHO inayorudia kujenga kipande cha kilometa 33 kinachoanzia kijiji cha Misigiri hadi Shelui wilayani Iramba.