Subscribe:

search

.

Thursday 9 August 2012

HATIMAYE MALAWI YAANZA KUONDOA MAJESHI YAKE KATIKA KINGO ZA ZIWA NYASA




Siku chache baada ya Serikali ya Tanzania kupitia kwa waziri wake wa mambo ya nje Mh. Bernad Membe kuitaka Serikali ya Malawi kuondoa majeshi na kampuni zinazofanya utafiti wa gesi kwenye ziwa Nyasa ukanda wa Tanzania wakidai kuwa ziwa hilo ni la kwao lote wameanza kufanya hivyo na kuondoka taratibu ukanda huo. Kwa mujibu wa mkuu wa mkoa wa Mbeya Bw. Abbas Kandoro alisema kuwa kwa sasa eneo hilo hali ni shwari kwani

makampuni, ndege na askari wa malawi waliokuwa wakiendesha shughuli zao kwenye eneo la Tanzania wametii amri na kuondoka kwenye eneo hilo hivyo wananchi wasiwe na shaka bali waendelee na kazi zao za kila siku kwenye ziwa hilo, Mbali na Waziri Membe, viongozi wengine waliozungumzia mgogoro huo na

kuitaka Malawi iache uchokozi ni Waziri wa Ushirikiano wa Afrika

Mashariki, Samuel Sitta na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Mambo ya

Nje, Ulinzi na Usalama, Edward Lowassa.
Chanzo: ThisDayMagazine

0 comments: