Subscribe:

search

.

Tuesday 14 August 2012

HAYA HAPA MABAKI YA NDEGE ZA UGANDA




Mabaki ya Helikopta mbili za Uganda ambazo ziliripotiwa kutoweka siku ya Jumapili zimepatikana mashambani nchini kenya.
Kanali Cyrus Oguna ambae ni msemaji wa jeshi la Kenya amesema hatma ya watu 14 waliokuwemo ndani ya chombo hicho haijulikani.
Ndege hizo mbili zilikuwa ni sehemu ya vifaa vilivyokuwa vikipelekwa nchini Somalia kuongezea nguvu kikosi cha umoja wa Afrika kilichoko huko.

Helikopta ya tatu ambayo pia ilikuwa katika msafari huo ilitua kwa ghafla katika eneo la mlima Kenya siku ya Jumapili.

Kanali Oguna amesema wote waliokuwa katika helikopta hiyo ya tatu waliokolewa.

Ni helikopta moja peke yake ndio faulu kutua vizuri na kuongeza mafuta katika mji wa Garissa ulioiko kaskzzini mwa Kenya.

Helikopta hizo nne ambazo zimetengezezwa Urusi ziliondoka siku ya Jumapili Uganda zikelekea Somalia kabla ya kukumbwa na mkasa huo.

Masalia ya helikopta hizo mbili ambazo awali ziliripotiwa kutoweka zilionekana juu ya mlima Kenya na maafisa wa Shirika la Wanyama pori, limeripoti gazeti la Daily Nation la Kenya.

Msemaji wa jeshi Kanali Oguna ameimbia BBC kwamba kikosi cha jeshi la Kenya linaelekea katika eneo hilo la Mlima Kenya , ambao ndio mlima wapili kwa urefu ,afrika.

Afisa huyo amefafanua kwamba moja ya helikopta hizo imeharibika kabisa ilhali ya pili imeharibika kiasi.

Helikpta hizo zilikuwa zinaelekea nchini Somalia kuongezea nguvu vikosi vya Umoja wa Afrika ambavyo vinajitayarisha kuvamia mji wa Kismayo na kuwafurusha wapiganaji wa Al Shabaab toka mji huo ambyo ndio ngome yao kuu.
Chanzo:mjengwablog.com

0 comments: