Subscribe:

search

.

Thursday 18 October 2012

MWANAMKE MSHIRIKINA AONYESHA NGOZI YA MTOTO WA MIAKA MIWILI

Mwanamke aliyejitambulisha kwa jina la Belikumana Lugome(48), Mkazi wa Kijiji cha Parangu Songea Mkoani Ruvuma amekiri kujihusisha na imani za kishirikina na kukabidhi sehemu ya madawa aliyokuwa akiyatumia kwa Mganga wa Jadi aliyefahamika kwa jina la Jesca Ndembo Mkazi wa Iyunga Mkoani Mbeya.

Mwanamke huyo alifika kwa Mganga huyo wa jadi Oktoba 12 mwaka huu, majira ya saa 8 mchana alipokwenda hapo kwa nia ya kumwangalia shangazi yake aliyekuwa akitibiwa na Mganga huyo.

Aidha imedaiwa kuwa shangazi yake huyo alirogwa na nduguye na mshirikina huyo kukiri kwamba ndiye alisababisha upasuaji wa tumbo lake mara mbili na kutakiwa apasuliwe tena na kama asingewahi angeuawa kwa siku za hivi karibuni.

Bi. Lugome amekiri kujihusisha na matukio ya ajali 15 mkoani Ruvuma na kusababisha vifo vya watu 15 katika ajali hizo.

Aidha alionesha sehemu ya vifaa ambavyo alikuwa akivitumia katika ushirikina ikiwemo ngozi ya mtoto wa miaka miwili.

Hata hivyo amesema kuwa yeye aliupata uchawi huo kutoka kwa Waganga mbalimbali Mkoani Ruvuma na kwamba hapendi hali hiyo kwani haina faida yoyote. 

0 comments: