Subscribe:

search

.

Thursday 18 October 2012

SHAMBULIO LA GURUNETI LAUA WATATU MOMBASA

 Maafisa wa polisi wa Kenya wakilinda nyumba katika kitongoji cha Likoni mjini Mombasa baada ya uvamizi wa polisi tarehe 17 Oktoba. [Na Stringer/AFP]
Maafisa tisa wa polisi walijeruhiwa katika shambulio la guruneti wakati wa uvamizi dhidi ya ugaidi katika eneo  la Mombasa  Kenya.
Watuhumiwa wawili wa ugaidi waliuliwa wakati wa uvamizi huo, na mmoja wa maafisa wa polisi waliojeruhiwa alifariki baadaye kutokana na majeraha akiwa hospitali.
 Police kutoka Kitengo cha Kupambana na Ugaidi walikuwa wanajaribu kuwakamata watuhumiwa wa ugaidi wakati wafuasi wa al-Shabaab walipowarushia guruneti, alisema Mkuu wa Polisi wa Mkoa wa Pwani Aggrey Adoli.
Alisema kuwa kabla ya hapo polisi walikuwa wamemtia mbaroni mshukiwa moja huko Changamwe ambaye aliwaongoza hadi kwenye nyumba.
"Tulipofika nyumbani hapo, wale waliokuwemo ndani walikataa kufungua na badala yake [mmoja wao], aliwarushia guruneti maafisa, na kumuua mwenzao na kuwajeruhi maofisa wetu. Baadaye aliuliwa wakati wa kutupiana risasi," Adoli alisema.
Polisi walipata bastola moja, bunduki aina ya AK-47, maguruneti mawili na risasi 15, kwa mujibu wa Adoli. Aliongeza kuwa ukamataji zaidi utafanywa pale askari watakapofanya juhudi za kupambana na ugaidi.

0 comments: