Subscribe:

search

.

Wednesday 17 October 2012

WANAFUNZI WASHIRIKI KUNAWA MIKONO


Mwanafunzi wa shule ya Mwenge akimuonyesha mwalimu wake (aliyeshika jagi) namna alivyofundishwa kunawa mikono.

ZAIDI ya Wanafunzi 300 kutoka shule nne za jijini Dar es Salaam, jana waliadhimisha Siku ya Kunawa mikono katika viwanja vya Posta, Kijitonyama, ambayo hufanyika Oktoba 15, kila mwaka huku kwa wanafunzi hao wakiadhimisha jana katika viwanja hivyo.

Wanafunzi hao walikutana katika viwanja hivyo kuanzia saa nne za asubuhi, huku mgeni rasmi akiwa ni Mratibu wa Tiba wa Manispaa ya Kinondoni, Sirila Mwanisi.

Katika maadhimisho hayo, wanafunzi hao walifundishwa jinsi ya kukabiliana na uchafu wakati wote, sambamba na unawaji wa mikono kabla na baada ya kula.

Akizungumza katika viwanja hivyo jana, Sirila alisema, kuwa, ni vyema watu wakajenga utamaduni wa kujitunza kwa wakati wote, ili wakabiliane ba maradhi yanayoweza kuepukika, vikiwano vijidudu vinavyosababisha magonjwa ya tumbo na kipindupindu.

Alisema kwamba watoto wadogo ndio wapo kwenye hatari zaidi, hivyo ni lazima wazazi na walezi pamoja na jamii husika kuwaelimisha kwa ajili ya kuwaweka katika mazingira mazuri.
“Watoto lazima waelimishwe namna ya kunawa mikono kabla na baada ya kula, maana ndio njia pekee ya kukabili vijidudu vya aina mbalimbali, ukiwamo ugonjwa wa kipindipindu ambao ndio hatari zaidi ndani na baadhi ya nchi za Afrika.

“Serikali kwa kushirikiana na asasi mbalimbali tunaamini tutafanikisha usafi wa unawaji wa mikono kwa ajili ya afya njema, ukizingatia kwamba ndio njia ya kufanikisha maisha bora kwa namna moja ama nyingine, hasa wote tukiwa na afya njema,” alisema Sirila.

Maadhimisho hayo ya siku ya kunawa yameandaliwa na Kampuni ya PCB WITNA na kudhaminiwa na sabuni ya Protex kwa ajili ya kukutanisha wanafunzi wa shule za Msingi Shikilango, Kijitonyama Kisiwani, Mapambano, Mwangaza na Mwenge.

Mgeni rasmi ambaye ni Mratibu wa Tiba wa Manispaa ya Kinondoni, Sirila Mwanisi akizungumza katika maadhimisho ya Siku ya Kunawa mikono katika viwanja vya Posta, Kijitonyama, ambayo hufanyika Oktoba 15, kila mwaka huku kwa wanafunzi hao wakiadhimisha siku hiyo jana katika viwanja hivyo.


Wanafunzi ya 300 kutoka shule za Msingi Shekilango, Kijitonyama Kisiwani, Mapambano, Mwangaza na Mwenge wakionyesha mfano wa kunawa mikono mara baada ya kupewa somo.

0 comments: